*FAHAMU UMUHIMU WA DCP KWA MIFUGO.* DCP=Dicalcium Phosphate ✅*DCP ni nini ?* DCP ni mchanganyiko wa madini ya Calcium na Phosphorus. DCP husaidia wanyama wenye upungufu au maradhi yatokanayo na ukosefu wa madini haya ya Calcium na Phosphorus ✅FAIDA KWA KUKU: Huzuia kudonoana, kula mayai, maganda malaini, huimarisha maganda ya mayai, Pia husaidia utagaji wa mayai ✅FAIDA KWA WANYAMA WENGINE: Huzuia ng’ombe kuanguka, viungo dhaifu na huimarisha mifupa na kupunguza matatizo ya mifupa. 📞Dr Riziki Ngogo(DVM) ☎*AfyaMIFUGO Tz* 0763222500 afyamifugo@gmail.com afyamifugo.blogspot.com
_UFANISI WA KUKU_ Fahamu kuwa, kwa kawaida kuku hunyonyoka manyoya na kuota manyoya mapya katika vipindi tofauti vya ukuaji wa kuku. *_Moulting_* Kunyonyoka manyoya na kubadilisha manyoya mapya hutokea kuku akiwa na umri wa kianzia wiki ya 4-5, wiki ya 8, Wiki ya 13, Wiki ya 20. Pia angalau mara moja kwa kila mwaka akifikia umri wa utagaji. Visababishi vingine vinavyochangia kunyonyoka manyoya na kuota manyoua mapya ni pamoja na _mabadiliko na upungufu wa chakula, mabadiliko ya kimsimu ya hali ya hewa, mabadiliko ya ghafla ya mwanga_ n.k Tambua kuwa kunyonyoka manyoya kunaweza kuathiri ufanisi wa kuku katika ukuaji/kuongezeka uzito na utagaji, hivyo unashauriwa kufanya yafuatayo, _1. Punguza stress kwa kuku._ _2. Tumia chakula bora chenye protein ya kutosha._ _3. Epuka mabadiliko ya ghafla kwenye mwanga, chakula n.k._ ●By Dr Riziki Ngogo 0763222500 #ReSta AgroVET #FARMERS Platform # INTERCHICK- ...