SABABU ZINAZOFANYA WAFUGAJI/WAJASIRIAMALI WENGI, KUSHINDWA KUFIKIA MALENGO?* 1. *MAARIFA YA KUTOSHA/ UJUZI SAHIHI.* Watu Wengi wanakimbilia ufugaji/kilimo baada ya kuona majirani na marafiki zao wamepata mavuno bora na yenye faida. Watu wa aina hii hawatengi muda wao wa kujifunza kuhusu mienendo ya soko na mahitaji na uzalishaji wa bidhaa na mazao ya mifugo.
_UFANISI WA KUKU_ Fahamu kuwa, kwa kawaida kuku hunyonyoka manyoya na kuota manyoya mapya katika vipindi tofauti vya ukuaji wa kuku. *_Moulting_* Kunyonyoka manyoya na kubadilisha manyoya mapya hutokea kuku akiwa na umri wa kianzia wiki ya 4-5, wiki ya 8, Wiki ya 13, Wiki ya 20. Pia angalau mara moja kwa kila mwaka akifikia umri wa utagaji. Visababishi vingine vinavyochangia kunyonyoka manyoya na kuota manyoua mapya ni pamoja na _mabadiliko na upungufu wa chakula, mabadiliko ya kimsimu ya hali ya hewa, mabadiliko ya ghafla ya mwanga_ n.k Tambua kuwa kunyonyoka manyoya kunaweza kuathiri ufanisi wa kuku katika ukuaji/kuongezeka uzito na utagaji, hivyo unashauriwa kufanya yafuatayo, _1. Punguza stress kwa kuku._ _2. Tumia chakula bora chenye protein ya kutosha._ _3. Epuka mabadiliko ya ghafla kwenye mwanga, chakula n.k._ ●By Dr Riziki Ngogo 0763222500 #ReSta AgroVET #FARMERS Platform # INTERCHICK- ...